Pages

Wednesday 14 March 2018

ASKOFU KKKT KUTEMBEA KWA MIGUU KILOMETA 340


 
Askofu wa dayosisi ya Kusini Mashariki ya Ziwa Victoria (Shinyanga na Simiyu), Dk. Emmanuel Makala ataweka rekodi katika utumishi wake kutokana na mpango wake wa kutembea kilometa 340 kwa lengo la kuujenga Ufalme wa Mungu.

Dk. Makala ataanza matembezi hayo ya majuma mawili machi 18 katika usharika wa Neema Lamadi na kumaliza Aprili 1 katika usharika wa Agape uliopo kahama.

Matembezi ya Askofu huyo yanalenga kukusanya fedha, Zaidi ya shilingi milioni 120 za maendeleo ya misioni za dayosisi hiyo ambayo inakabiliwa na changamoto mbalimbali kutokana na kuwa ni eneo ambalo lina mauaji ya albino na vikongwe.

Mojawapo ya mambo atakayofanya katika matembezi hayo ya miguu ni pamoja na kuendeleza kazi ya injilli, kukemea mauaji ya albino na kusisitiza watu kufanya kazi kwa bidii.

KILA LA KHERI ASKOFU.

SOURCE: UPENDO MEDIA

No comments:

Post a Comment