USHIRIKINA: MDADA AUNGUZWA KWA MOTO NA WAGANGA ILI APATE UJAUZITO


RORYA, MARA: Jeshi la Polisi linawashikilia waganga wa jadi wawili kwa tuhuma za kumuunguza kwa moto Emiliana Thomas mwenye tatizo la kutopata ujauzito

Waganga hao walimwambia Emiliana kuwa ili apate mtoto ni mpaka kuku amwagiwe mafuta ya taa na ateketezwe kwa moto huku mama huyo akiwa amemshikilia mikononi

Kamanda wa Polisi, Henry Mwaibambe alisema waganga hao walimweleza mwanamke huyo kuwa anasumbuliwa na mashetani ndani ya tumbo na ndio yanayomfanya asizae, hivyo kuku akiteketea mikononi mwake atakuwa ameondokana na mashetani

Aidha, Mwaibambe amesema hali ya mama huyo ni mbaya na anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Kowak wilayani humo

TUMWAMINI MUNGU JAMANI. Neno lake linasema kuwa TUNAPOTEA KWA KUKOSA MAARIFA. 

SOURCE: JAMIIFORUMS

0 comments:

Copyright © 2018 iCHURCH Magazine