SERIKALI YAFUNGIA KANISA KWA TUHUMA ZA KUTENGENEZA FEDHA ZA MIUJIZA




Serikali nchini Botswana imelifungia kanisa la Nabii Shepherd Bushiri kwa kile kinachodaiwa kuwa anatengeneza “fedha za ajabu”.

Mtumishi huyo alishutumiwa mwaka uliopita baada ya kubainika kuwa alikuwa akiwatoza kati ya dola 80 hadi 2000 wafuasi wake walikokuwa wakitaka kuhudhuria chakula cha jioni. Nabii Bushiri ni maarufu kwa mtindo wake wa Maisha ya kifahari huku akiwa na wafuasi wengi katika kanisa lake.

Bushiri ana wafuasi wengi na alifanikiwa kujaza watu katika mkesha wa mwaka mpya kwenye uwanja wa mpira wa FNB ambao ulitumika kwenye fainali za kombe la dunia mwaka 2010 nchini Afrika ya kusini. Pia mhubiri huyo ana wafuasi wengi kwenye mitandao ya kijamii.

Kwa mujibu wa chombo cha habari cha Malawi 24, kanisa hilo lilipinga uamuzi huo mahakamani na limekata rufaa ya kutaka kuendelea na huduma yake. 

Hata hivyo waziri wa mambo ya ndani wa Botswana, Edwin Batshu alitangaza Aprili mwaka jana kwamba Nabii Bushiri ambaye sasa anaishi Afrika ya kusini, atahitaji VISA ili kuingia nchini humo, licha ya raia kutoka Malawi kutohitaji kibali. 
Serikali ya nchi hiyo imetangaza kuwa kanisa hilo litafungwa huku vyombo vya habari vikielekeza kuwa kibali cha kuendesha kanisa hilo kimefutwa. 


0 comments:

Copyright © 2018 iCHURCH Magazine