UONGOZI WA FACEBOOK WAUFUNGA UKURASA WA MASHUJAA WA KRISTO (Warriors for Christ)


NEW YORK:

Uongozi wa mtandao wa kijamii wa FACEBOOK umeamua kuuondoa ukurasa uliokuwa ukimilikiwa na kikundi cha waumini waliokuwa wakijiita mashujaa wa kristo (warriors for Christ). 

Ukurasa huo uliokuwa na wafuatiliaji Zaidi ya laki mbili, ukiendeshwa kwa maudhui ya kupinga dhambi ulifungwa hivi karibuni baada ya kudaiwa kuwa na matumizi ya lugha kali na chuki.

Ilielezwa kuwa asili ya ukurasa huo ilitokana na waumini wa huduma ya kikristo iliyoko West Virginia nchini Marekani.

Uongozi wa mtandao huo ulieleza kukerwa na tabia ya wafuatiliaji wa ukurasa huo kutoa lugha za kukejeli na kupinga huduma za utoaji mimba na vyama vinavyotetea mahusiano ya jinsia moja.

Maneno ya wafuatiliaji hao yaliambatanishwa na ujumbe wa video wa mchungaji wa huduma yao, Rich Penkoski kuhusu kupinga vitendo hivyo vilivyotafsiriwa kama uchochezi hivyo Facebook kuufunga ukurasa huo.

Inaelezwa kuwa ukurasa huu uliwahi kufungwa kwa mara ya kwanza mwezi Disemba 2017 lakini ulifunguliwa muda mchache baada ya watu wengi kutaka uongozi wa Facebook kutafakari upya maamuzi yao na sasa umefungwa tena.

0 comments:

Copyright © 2018 iCHURCH Magazine