WAPINGA KRISTO WAZIDI KUSUMBUA VYUONI MAREKANI

NEW YORK

Kundi la watu wasioamini Mungu wanaotambulika kama ATHEIST, wamekitaka chuo kimoja nchini marekani kuondoa misalaba iliyopo katika majengo yake.

Ilielezwa kuwa chuo cha New Mexico kilikuwa na misalaba kadhaa ikionesha uwepo wa Imani ya Kikristo lakini kundi hilo lilishinikiza kuondoa likidai kuwa kwasababu chou hicho sio cha kidini, sio sahihi kuweka alama za misalaba.

Wapinga Mungu hao kupitia uongozi wake walituma barua kwa raisi wa chuo hicho bwana Kelvin Sharp, wakitaka kusiwepo na alama zozote za kidini kwenye maeneo ya chou hicho kwasababu yanamilikiwa na umma.
alama ya msalaba ukiwa mlangoni
mwa ofisi za chuo hicho

“Tunafahamu kuwa chou cha New Mexico Junior kina misalaba kadhaa inayoonekana. Tunaelewa kuwa kuna misalaba kwenye sehemu za mapokezi n ahata ofisi ya mhasibu.” Barua ilisomeka hivyo.
Barua hiyo ilieleza kuwa kuweka misalaba kwenye maeneo ya umma ni kinyume na katiba ya nchi hiyo.

SOURCE: UPENDO MEDIA

0 comments:

Copyright © 2018 iCHURCH Magazine